08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Tano, hatunabudi kuchukia maovu na dhulma<br />

wanazofanyiwa wanyonge na madhaifu wengine katika jamii na<br />

kuwa tayari kuondoa maovu na dhulma kwa mikono yetu pale<br />

tunapoweza. Na pale ambapo hatuna uwezo wa kutumia mikono,<br />

tutoe makemeo, vinginevyo tuingie “pangoni Hira” tutafute<br />

msaada wa Allah (s.w).<br />

Sita, hatunabudi kujipamba na tabia njema kwa kadiri<br />

iwezekanavyo. Mtu mwema hutambulika na kukubalika kwa watu<br />

kwa urahisi.<br />

Saba, hatunabudi kuimarisha uchumi, kwani uchumi ndio<br />

nyenzo kuu ya kuusimamisha Uislamu katika jamii.<br />

Nane,Katika kuchagua viongozi wa jamii hatunabudi<br />

kuzingatia historia zao pamoja na kuzingatia sifa nyingine za<br />

kiongozi bora.<br />

Maandalizi ya Kimafunzo<br />

Ni maandalizi yaliyompitia Mtume (s.a.w) pale alipoanza<br />

kuletewa wahyi na Malaika Jibril (a.s). Maandalizi haya<br />

tunayapata katika Qur-an katika wahay wa mwanzo mwanzo<br />

kumshukia Mtume (s.a.w) katika Suratul ‘Alaq (96:1-5), Suratul-<br />

Muzzammil (73:1-10) na Suratul-Muddaththir (74:1-7).<br />

(i) Suratul-A’laq (96:1-5)<br />

“Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba<br />

Aliyemuumba mwanaadamu kwa a’laq. Soma na Mola<br />

wako ni karimu sana. Ambaye amefundisha kwa<br />

msaada wa kalamu. Amemfundisha mwanaadamu<br />

mambo aliyokuwa hayajui.” (96:1-5)<br />

49

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!