Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Utangulizi:<br />
Sura ya Tatu<br />
MWANAHARAKATI WA KIISLAMU<br />
Dai’ah au Mwanaharakati ni Muislamu anayefanya jitihada<br />
za makusudi za kusimamisha Uislamu katika jamii.<br />
Da’awah au kazi ya kulingania Uislamu ndiyo kazi ya Mitume<br />
wote hivyo mitume wote walikuwa Wanaharakati. Kila Muumini<br />
wa kweli anawajibika kuwaiga mitume katika kazi ya Da’awah,kazi<br />
ya kuwaita watu kwenye Uislamu ili waufuate vilivyo na<br />
kuusimamisha katika jamii.Katika Hija ya kuaga (Hijjatul-Wadaa),<br />
Mtume Muhammad (s.a.w) alimuagiza kila Muislamu kuufikisha<br />
ujumbe wa Uislamu kwa kadri ya uwezo wake angalau aya moja<br />
anayoifahamu.Mwishoni mwa Khutba yake alisema:<br />
“Na afikishe aliyekuwepo kwa yule asiyekuwepo.Kwani<br />
watu wengi wanaofikishiwa ujumbe wanaweza kuwa wenye<br />
kuufuata (wenye kuuzingatia) kuliko walioupata moja kwa<br />
moja kwa mtoaji ujumbe”.<br />
Kutokana na maelezo hayo ni dhahiri kuwa kila Muislamu<br />
anawajibika kuufikisha ujumbe wa Uislamu kwa wengine kwa<br />
kadri ya uwezo wake. Akianzia na watu wa nyumbani kwake, jamaa<br />
zake, rafiki zake na kisha jamii yake kuanzia ngazi ya mtaa hadi<br />
taifa na Mataifa.<br />
Mitume wa Allah (s.w) hawakuifanya kazi hii kinadharia tu,<br />
bali walikuwa katika mstari wa mbele katika utekelezaji wake.<br />
Waliwavutia wafuasi wao si kwa maneno tu, bali tabia zao na<br />
mienendo yao mizuri iliathiri jamii zao kwa kiasi kikubwa. Hivyo<br />
yeyote yule aliyeitikia wito wa kuifanya kazi hii takatifu ya<br />
62