08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Utangulizi:<br />

Sura ya Tatu<br />

MWANAHARAKATI WA KIISLAMU<br />

Dai’ah au Mwanaharakati ni Muislamu anayefanya jitihada<br />

za makusudi za kusimamisha Uislamu katika jamii.<br />

Da’awah au kazi ya kulingania Uislamu ndiyo kazi ya Mitume<br />

wote hivyo mitume wote walikuwa Wanaharakati. Kila Muumini<br />

wa kweli anawajibika kuwaiga mitume katika kazi ya Da’awah,kazi<br />

ya kuwaita watu kwenye Uislamu ili waufuate vilivyo na<br />

kuusimamisha katika jamii.Katika Hija ya kuaga (Hijjatul-Wadaa),<br />

Mtume Muhammad (s.a.w) alimuagiza kila Muislamu kuufikisha<br />

ujumbe wa Uislamu kwa kadri ya uwezo wake angalau aya moja<br />

anayoifahamu.Mwishoni mwa Khutba yake alisema:<br />

“Na afikishe aliyekuwepo kwa yule asiyekuwepo.Kwani<br />

watu wengi wanaofikishiwa ujumbe wanaweza kuwa wenye<br />

kuufuata (wenye kuuzingatia) kuliko walioupata moja kwa<br />

moja kwa mtoaji ujumbe”.<br />

Kutokana na maelezo hayo ni dhahiri kuwa kila Muislamu<br />

anawajibika kuufikisha ujumbe wa Uislamu kwa wengine kwa<br />

kadri ya uwezo wake. Akianzia na watu wa nyumbani kwake, jamaa<br />

zake, rafiki zake na kisha jamii yake kuanzia ngazi ya mtaa hadi<br />

taifa na Mataifa.<br />

Mitume wa Allah (s.w) hawakuifanya kazi hii kinadharia tu,<br />

bali walikuwa katika mstari wa mbele katika utekelezaji wake.<br />

Waliwavutia wafuasi wao si kwa maneno tu, bali tabia zao na<br />

mienendo yao mizuri iliathiri jamii zao kwa kiasi kikubwa. Hivyo<br />

yeyote yule aliyeitikia wito wa kuifanya kazi hii takatifu ya<br />

62

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!