08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Na namna hii tumemfanyia kila Nabii maadui (na ni)<br />

mashetani katika watu na majini. Baadhi yao<br />

wanawafunulia wenziwao maneno ya kupamba-pamba ili<br />

kuwadanganya (na kuwapoteza). Na kama Mola wako<br />

angalipenda wasingalifanya hayo. Basi waache na<br />

uwongo wao. (6:112)<br />

Katika Qur’an tunajifunza kuwa Shetani ni katika watu na<br />

majini ambao huwalaghai watu kwa maneno ya kupamba pamba ili<br />

waache kuufuata Uislamu kama ulivyoelekezwa katika Qur-an na<br />

mafundisho ya Mtume (s.a.w) na badala yake wafuate njia ya hao<br />

mashetani (matwaghuuti). Tunatahadharishwa katika Qur’an<br />

kuwa wale wasioamini Akhera watatekwa nyara na mashetani,<br />

watawafanya marafiki,watawatii na kufuata utaratibu wa maisha<br />

waliowapambia. Tunafahamishwa katika aya hizi kuwa dawa ya<br />

kumwepuka Shetani ni kufuata hukumu zote za Qur-an, yaani<br />

kuendesha maisha yote kwa mujibu wa Qur-an na Sunnah.<br />

Endapo Muislamu atatokea kuteleza au kuhisi kuteleza kidogo na<br />

kutoka nje ya Qur-an na Sunnah, basi mara tu anapogundua hivyo<br />

ajikinge kwa Allah (s.w) na Shetani na arejee haraka katika njia<br />

iliyonyooka kama tunavyoelekezwa katika Qur-an:<br />

Na kama wasiwasi wa shetani ukikusumbua, basi jikinge<br />

kwa Mwenyezi Mungu. Bila shaka yeye ndiye asikiaye na<br />

ajuaye.(7:200)<br />

159

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!