Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
wanashirikiana na utawala wa Kitwaghut katika kuzima harakati za<br />
kulingania na kusimamisha Uislamu katika jamii.<br />
4. Kulingania kwa Hekima<br />
Hekima ni kipengele cha tabia njema chenye maana pana.<br />
Hekima kwa ujumla ni kufanya jambo la sawa sawa kwa namna ya<br />
sawa sawa kwa wakati wa sawa sawa na katika mazingira ya sawa<br />
sawa katika kuendea lengo husika. Kwa mnasaba wa kulingania<br />
Uislamu kwa lengo la kuusimamisha katika jamii hekima itakuwa<br />
imetumika pale:<br />
(1) Uislamu utakapolinganiwa kwa usahihi wake kwa kutumia<br />
mtaala wa Qur’an na Sunnah.<br />
(2) Kisha ukafundishwa kwa kutumia mbinu stahiki<br />
zinazolandana na mwongozo wa.Qur’an na Sunnah.<br />
(3) Kisha ukafundishwa kwa kuzingatia wakati uliopo, wakati<br />
wa sayansi na teknolojia, wakati wa utandawazi, n.k.<br />
(4) Na kisha ukazingatia mazingira yaliyopo, ikiwa ni pamoja na<br />
kujua historia ya Uislamu wa watu wa eneo husika; maadui<br />
wa Uislamu na mbinu zao dhidi ya Uisiamu, mila na desturi<br />
za watu unao walingania, umri wao, kiwango chao cha elimu<br />
ya mazingira na elimu ya mwongozo n.k.<br />
Ni vema kusisitiza kuwa hekima si woga au kuchelea<br />
matatizo au kuepa majukumu. Mara nyingi wanafiki wamesingizia<br />
kutumia hekima, kumbe wanaogopa au wanachelea kukabiliana na<br />
magumu au wanaepa majukumu yanayo wakabili katika mchakato<br />
wa kusimamisha Uislamu katika jamii. Ni kweli kwamba kazi ya<br />
kulingania na kusimamisha Uislamu katika jamii si jambo jepesi,<br />
bali ni jambo linalohitaji ujasiri, kujitoa muhanga na subira kama<br />
Allah (s.w) anavyotukumbusha mara kwa mara katika Qur’an<br />
(rejea 2:214; 3:142; 9:16; 47:31)<br />
128