08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Kiongozi muadilifu ni yule anayechunga haki za watu<br />

anaowaongoza. Yeye ni mchunga na mgawaji wa haki. Hana budi<br />

kuhakikisha kuwa yeye mwenyewe hachukui haki zake mpaka<br />

ahakikishe kuwa kila mtu amepata haki yake. Mtume (s.a.w)<br />

aliwaamuru wale aliowapa kazi ya uongozi wasivae kivazi kizuri<br />

zaidi kuliko watu wengine, wasifunge milango yao wakati watu<br />

wanawahitajia haki zao au wanataka kutoa madukuduku yao.<br />

Kiongozi wa Kiislamu anatakiwa awe muaminifu na mkweli<br />

na asithubutu kujilimbikizia mali kwa kutumia madaraka yake ya<br />

uongozi. Amir au kiongozi wa juu wa Serikali ya Kiislamu<br />

anatakiwa achukue mshahara au posho kutoka kwenye mfuko wa<br />

serikali (Baitul-Mali) kiasi kile tu kinachotosheleza mahitaji<br />

muhimu ya chakula, mavazi na makazi kwa yeye mwenyewe na<br />

familia yake. Kiongozi wa Kiislamu anatakiwa akumbuke daima<br />

kuwa uongozi katika Uislamu si kitega uchumi kama ulivyo<br />

uongozi wa Kitwaghuti. Mtume Muhammad (s.a.w) ambaye ndiye<br />

kiongozi wa Ummah huu wa mwisho na kiigizo chetu kwa<br />

mwenendo na uongozi wake bora, aliishi maisha rahisi.<br />

Abu bakar (r.a) aliyechaguliwa kushika uongozi wa Umma<br />

wa Kiislamu mara baada ya kutawafu Mtume (s.a.w), alifuata<br />

nyayo za Mtume (s.a.w) kwa kila kitu. Maisha yake yalikuwa rahisi<br />

mno. Umar (r.a) aliyechaguliwa kuwa kiongozi wa serikali ya<br />

Kiislamu baada ya Abu Bakar alifuata vyema nyayo za Mtume<br />

(s.a.w) na Abu Bakar. Pamoja na kuwa Umar alikuwa kiongozi wa<br />

dola kubwa ya Kiislamu iliyoenea mashariki ya kati yote na<br />

kupanuka hadi Spain, aliishi maisha rahisi sana. Umar (r.a)<br />

alikuwa na kawaida ya kuzunguka usiku ili kujua matatizo ya watu<br />

wake.<br />

Kinyume chake viongozi wa Kitwaghuti, huchukua madaraka<br />

ya uongozi wanayopewa na jamii zao kama kitega uchumi chao kwa<br />

ajili ya kujinufaisha wao binafsi. Huifuja watakavyo na humpa<br />

194

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!