08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

“Kwa yakini Mwenyezi Mungu anawapenda wale wanaopigana<br />

katika njia yake safu safu (mkono mmoja) kama kwamba wao ni<br />

jengo lililokamatana barabara.” (61:4)<br />

Kundi hili litapatikana pale tu Waislamu walioamua<br />

kujiingiza katika kazi ya kupigania dini ya Allah (s.w)<br />

watakapokamatana baraabara kwa ushirikiano, umoja, udugu na<br />

upendo. Mshikamano au mkamatano wa aina hii ni muhali<br />

kupatikana pasi na kila mwanakundi kuzingatia na kutekeleza<br />

yafuatayo:<br />

(a) Kuwa na lengo moja tu.<br />

(b) Kuwafanyia wema wanakundi na<br />

(c) Kutowafanyia mabaya wanakundi.<br />

(a) Kuwa na lengo moja tu<br />

Kila mlinganiaji hana budi kufahamu vyema kuwa lengo lililo<br />

mbele yake ni kuhakikisha kuwa dini ya Allah (s.w) inasimama<br />

katika jamii na kuwa juu ya dini zote kama lengo hili<br />

lilivyobainishwa katika Qur-an:<br />

“Yeye (Allah) ndiye aliyemtuma Mtume wake kwa uongofu<br />

na dini ya haki ili kuifanya ishinde dini zote ijapokuwa<br />

washirikina watachukia.” (9:33, 61:9)<br />

Maana ya Uislam kuwa juu ya dini nyingine zote ni kwamba<br />

pamoja na kuwepo taratibu nyingine za maisha katika jamii,<br />

utaratibu wa maisha aliouweka Allah (s.w) kupitia kwa Mitume<br />

yake, yaani Uislamu, ndio pekee utakaofuatwa na Waislamu katika<br />

kuendesha maisha yao ya kibinafsi na ya kijamii.<br />

85

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!