08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Pia katika aya hii (49:12) tunaonywa kuwa tujiepushe na<br />

kuwadhania watu vibaya na kupeleleza mambo ya watu. Haya<br />

nayo ni matunda maovu yanayofitinisha watu walioungana na<br />

kuwafarakanisha.<br />

(iii) Kudharauliana na Kutukanana<br />

Dharau na matusi ni miongoni mwa maovu yanayovuruga<br />

mshikamano na upendo baina ya watu. Maovu haya yanakemewa<br />

katika aya ifuatayo:<br />

Enyi mlioamini! Wanaume wasiwadharau wanaume<br />

wenzao, huenda wakawa bora kuliko wao; wala wanawake<br />

wasiwadharau wanawake wenzao, huenda wakawa bora<br />

kuliko wao. Wala msitukanane kwa kabila, wala msiitane<br />

kwa majina mabaya (ya kejeli). Jina baya la kuambiwa mtu<br />

ni “asi” baada ya kuwa ni Muislamu. Na wasiotubu basi<br />

hao ndio madhalimu. (49:11).<br />

(iv) Kumchukia Muislamu pasina sababu ya msingi<br />

Ni katika uovu kumchukia Muislamu bila ya sababu ya msingi.<br />

Kupenda kwa Muislamu na kuchukia kwake watu kuwe kwa ajili ya<br />

Allah (s.w) tu.<br />

(v) Kuvunjiana heshima na kuzuliana<br />

Kuvunjiana heshima na kuzuliana ni miongoni mwa maovu<br />

ambayo husababisha chuki na uhasama baina ya watu.<br />

97

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!