08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Hapana shaka kuwa kundi la Harakati na Waislamu wote<br />

kwa ujumla watashikamana pamoja na kuwa umma mmoja<br />

endapo kila mmoja atakuwa na lengo la kusimamisha Uislamu<br />

katika jamii na endapo kila mmoja atajitahidi kuwatendea ndugu<br />

zake wema na kujitahidi kujiepusha na kuwatendea maovu. Baada<br />

ya kuwa Waislamu wameungana na kushikamana pamoja,<br />

pasitokee mtu wa kuwafarakanisha. Mwenye kuwafarakanisha<br />

Waislamu ni adui mkubwa mbele ya Allah (s.w) na anastahiki<br />

kupigwa vita kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatayo:<br />

Usamah bin Shariik (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah<br />

amesema: “Yeyote yule atakayejitokeza kuwagawanya<br />

Waislamu, mkateni kichwa chake”. (Nisai).<br />

Pia Muislamu haruhusiwi kujitenga na ummah wa Kiislamu<br />

kwa vyovyote vile itakavyokuwa. Mwenye kujitenga na Ummah wa<br />

Kiislamu atakuwa amejitenga na Uislamu hata kama ataendelea<br />

kuswali, kufunga, kuhiji, na kadhalika, kama tunavyojifunza katika<br />

Hadith zifuatazo:<br />

Ibn Abbas (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema:<br />

“Yeyote atakayeona jambo lisilompendeza kwa Kiongozi<br />

wake awe na subira, kwani hapana yeyote atakayejitenga na<br />

Jumuiya (Ummah) ya Kiislamu hata kiasi cha kimo cha<br />

kiganja cha mkono, ila akifa anakufa kifo cha wakati wa<br />

ujahili. (Bukhari na Muslim).<br />

Ibn Umar (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema:<br />

“Allah (s.w) hatawaunganisha wafuasi wangu (Waislamu)<br />

katika mambo ya upotofu, na mkono wa Allah uko juu ya<br />

watu walioshikamana; na atakayejitenga (na Ummah)<br />

atatengwa katika moto wa Jahannam.” (Tirmidh)<br />

98

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!