Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Hapana shaka kuwa kundi la Harakati na Waislamu wote<br />
kwa ujumla watashikamana pamoja na kuwa umma mmoja<br />
endapo kila mmoja atakuwa na lengo la kusimamisha Uislamu<br />
katika jamii na endapo kila mmoja atajitahidi kuwatendea ndugu<br />
zake wema na kujitahidi kujiepusha na kuwatendea maovu. Baada<br />
ya kuwa Waislamu wameungana na kushikamana pamoja,<br />
pasitokee mtu wa kuwafarakanisha. Mwenye kuwafarakanisha<br />
Waislamu ni adui mkubwa mbele ya Allah (s.w) na anastahiki<br />
kupigwa vita kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatayo:<br />
Usamah bin Shariik (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah<br />
amesema: “Yeyote yule atakayejitokeza kuwagawanya<br />
Waislamu, mkateni kichwa chake”. (Nisai).<br />
Pia Muislamu haruhusiwi kujitenga na ummah wa Kiislamu<br />
kwa vyovyote vile itakavyokuwa. Mwenye kujitenga na Ummah wa<br />
Kiislamu atakuwa amejitenga na Uislamu hata kama ataendelea<br />
kuswali, kufunga, kuhiji, na kadhalika, kama tunavyojifunza katika<br />
Hadith zifuatazo:<br />
Ibn Abbas (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema:<br />
“Yeyote atakayeona jambo lisilompendeza kwa Kiongozi<br />
wake awe na subira, kwani hapana yeyote atakayejitenga na<br />
Jumuiya (Ummah) ya Kiislamu hata kiasi cha kimo cha<br />
kiganja cha mkono, ila akifa anakufa kifo cha wakati wa<br />
ujahili. (Bukhari na Muslim).<br />
Ibn Umar (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema:<br />
“Allah (s.w) hatawaunganisha wafuasi wangu (Waislamu)<br />
katika mambo ya upotofu, na mkono wa Allah uko juu ya<br />
watu walioshikamana; na atakayejitenga (na Ummah)<br />
atatengwa katika moto wa Jahannam.” (Tirmidh)<br />
98