08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

kulingania Uislamu. Asiwe ni mwenye mashaka mashaka na wala<br />

asirudi nyuma kwa hali yoyote itakayokuwa mpaka mwisho wa<br />

uhai wake.<br />

(iv) Mwanaharakati anatakiwa awe tayari kupambana<br />

na magumu mbalimbali katika kuifanya kazi hii takatifu.<br />

Historia inatufahamisha wazi kuwa Mitume wa Allah (s.w) na wale<br />

walioamini pamoja nao walikabiliwa na magumu mbalimbali,<br />

lakini hawakukata tamaa. Bali walisubiri na walizidi kuwa imara na<br />

thabiti kila matatizo yalipoongezeka.Hii ndio tabia ya waumini wa<br />

kweli kama Allah (s.w) anavyobainisha katika Quran:<br />

Na waumini walipoyaona majeshi (ya makafiri) walisema:<br />

(Haya ndiyo aliyotuahidi Mwenyezi Mungu na Mtume wake<br />

(kuwa tutapata misukosuko kisha tutashinda). Mwenyezi<br />

mungu na Mtume wake wamesema kweli na jambo hili<br />

halikuwazidishia ila Imani na utii.(33:22)<br />

Pia Allah (s.w) anatukumbusha kuwa kamwe tusitarajie<br />

mafanikio ya kusimamisha Uislamu na kupata malipo ya Peponi<br />

pasina kuwa tayari kupambana na matatizo mbalimbali kama yale<br />

yaliyowasibu waliopita kabla yetu.<br />

Je! watu wanadhani wataachwa (wasitiwe katika<br />

misukosuko) kwa kuwa wanasema ((Tumeamini?} Basi<br />

ndiyo wasijaribiwe (wasipewe mitihani)? Hapana, bila<br />

shaka tuliwatia katika taabu wale waliokuwa kabla yao,na<br />

kwa yakini Mwenyezi Mungu atawatambulisha wale walio<br />

wakweli na atawatambulisha (wale walio) waongo.(29:2-3)<br />

73

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!