08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

yeyote wamtakaye kwa upendeleo mali ya jamii ambayo<br />

imepatikana kwa kukung’uta mifuko ya masikini. Muda mfupi<br />

baada ya kiongozi wa Kitwaghuti kukabidhiwa madaraka ya<br />

uongozi wa ngazi ya juu katika jamii, utamuona ana gari zuri jipya<br />

ana nyumba nzuri mpya na mabadiliko ya kila namna katika<br />

matumizi yake ya kimaisha pamoja na familia yake. Kama mambo<br />

yenyewe ni haya, kwa nini watu wengine katika jamii ya Kitwaghuti<br />

wasiupupie uongozi kwa hali na mali au kwa kufa na kupona? Kwa<br />

nini mtu aliyeonja uongozi katika serikali ya Kitwaghuti<br />

asing’ang’anie kubakia humo kwa gharama yoyote ile? Kwa nini<br />

mapinduzi ya mara kwa mara na mauaji yasitegemewe katika jamii<br />

za Kitwaghuti ambapo watu wanashindania uongozi kwa lengo la<br />

kujinufaisha wao binafsi na familia zao? Haya yote ni matunda<br />

machungu yanayotarajiwa katika jamii kutokana na uongozi<br />

uliokosa uadilifu.<br />

Kiongozi muadilifu hana budi kuhakikisha kuwa wanyonge<br />

katika jamii wanapata haki zao na wenye mali wanatoa haki za<br />

wanyonge. Abu Bakar, katika khutuba yake ya kwanza baada ya<br />

kuchaguliwa kuwa Khalifa wa kwanza wa Mtume (s.a.w) alisisitiza:<br />

“Mnyonge miongoni mwenu ni mwenye nguvu katika<br />

uongozi wangu mpaka apate haki zake; na mwenye nguvu<br />

miongoni mwenu atakuwa dhaifu katika uongozi wangu,<br />

mpaka akipenda Allah nichukue haki za watu<br />

anazodaiwa…......” 3<br />

Vile vile ni katika uadilifu kwa kiongozi kuhakikisha kuwa<br />

kila mtu mkosaji anahukumiwa kwa mujibu wa sharia bila ya<br />

upendeleo au uonevu wowote. Kiongozi hatamchelea yeyote katika<br />

kupitisha hukumu. Katika Uislamu watu wote ni sawa mbele ya<br />

sharia na hakuna aliye juu ya sharia hata akiwa Amir (Rais) wa<br />

nchi.<br />

(Prof: Shibli Muman al-Farooq - The life of<br />

Omar the Great uk.61)<br />

195

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!