08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Utangulizi:<br />

Sura ya Kwanza<br />

HAJA YA KUSIMAMISHA UISLAMU<br />

KATIKA JAMII<br />

Kusimamisha Uislamu katika jamii ndio lengo kuu la kuletwa<br />

Mtume(s.a.w) kama inavyobainika katika Qur’an:<br />

“Yeye (Allah) ndiye aliyemtuma Mtume wake kwa uongofu na<br />

dini ya haki (Uislamu) ili aijaalie kushinda dini zote, ijapokuwa<br />

watachukia washirikina.” (9:33, 61:9)<br />

Kwa mujibu wa aya hii ambayo imerudiwa katika sura mbili<br />

tofauti, lengo la kuletwa Mtume Muhammad (s.a.w), na mitume<br />

wote kwa ujumla, ni kuutawalisha Uislamu juu ya mifumo yote ya<br />

maisha katika jamii ya binaadamu.<br />

Katika kipindi cha miaka 23, Mtume (s.a.w) na waumini<br />

aliokuwa pamoja nao, walifanikiwa kufikia lengo hili na Allah (s.w)<br />

anashuhudia hili katika aya ifuatayo:<br />

Yeye ndiye aliyemtuma, (aliyemleta) Mtume wake kwa uwongofu na<br />

dini iliyo ya haki, ili aishindishe juu ya dini zote. Na Mwenyezi<br />

Mungu anatosha kuwa Shahidi”. (48:28).<br />

1

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!