Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
“Na ni nani asemaye kauli bora zaidi kuliko (yule) aitaye<br />
(watu) kwa Mwenyezi Mungu, (mwenyewe) akawa anafanya<br />
vitendo vizuri na kusema (kwa maneno yake na vitendo<br />
vyake) “Hakika mimi ni miongoni mwa Waislamu”. (41 :33)<br />
Kutokana na aya hii tunajlfunza kuwa mlinganiaji hanabudi<br />
kuwa na sifa za msingi zifuatazo:<br />
(i) Awe na ujuzi sahihi juu ya Uislamu<br />
(ii) Awe ni mfano wa kuigwa katika kuufuata Uislamu katika<br />
kukiendea kila kipengele cha maisha yake ya kibinafsi na ya<br />
kijamii kwa kadiri ya uwezo wake. Yaani mlinganiaji awe ni<br />
mwenye kujipamba na vipengele vyote vya tabia njema kama<br />
vilivyo ainishwa katika Qur’an na Sunnah<br />
Kwa ujumla, ili mlinganiaji aweze kuwaleta watu kwenye<br />
Uislamu kiasi cha kuwa tayari kuufuata na kuusimamisha katika<br />
jamii, hanabudi kujipamba na Sifa za Mwanaharakati<br />
zilizoainishwa katika Qur’an na Hadithi sahihi za Mtume (s.a.w)<br />
ambazo ni:<br />
Ujuzi sahihi juu ya Uislamu.<br />
Imani thabiti na kuwa na msimamo.<br />
Tabia njema ya kiutendaji.<br />
Lengo kuu la maisha liwe ni kusimamisha Uislamu katika<br />
jamii.<br />
Kutarajia malipo kutoka kwa Allah (s.w) tu .<br />
Kuwa na Hekima.<br />
Kuwa na Subira. (Rejea Sifa za Mwanaharakati<br />
sura ya tatu).<br />
Mlinganiaji wa Uislamu atakapoamua kulingania bila ya<br />
kujipamba na sifa stahiki zilizoorodhesha, si tu hatafanikiwa<br />
kuwashawishi watu kuwa Waislamu na kuwajengea ari na hamasa<br />
120