08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Tukirejea historia, tunaona kuwa Mtume Muhammad (s.a.w)<br />

alipata maandalizi ya aina mbili, Maandalizi ya Ki-il-hamu na<br />

Maandalizi ya kufunzwa na kuelekezwa moja kwa moja.<br />

Maandalizi ya Ki-il-hamu<br />

Ni maandalizi yaliyompitia Mtume (s.a.w) katika kipindi cha<br />

miaka 40 kabla ya kupewa Utume rasmi. Katika maandalizi haya<br />

hapana mafunzo rasmi yanayotolewa bali tunajifunza kutokana na<br />

matukio na mazingira kuwa palikuwa na mpango maalum<br />

uliopangwa kumuaanda Mtume(s.a.w). Ili tuone maandalizi haya<br />

hebu tuzingatie matukio machache katika maisha ya Muhammad<br />

(s.a.w) kabla ya kupewa Utume ikiwa ni pamoja na:<br />

(i) Kuzaliwa Makka katika kabila tukufu la Quraish<br />

(ii) Kupewa jina la Muhammad<br />

(iii) Malezi bora aliyoyapata<br />

(iv) Tabia njema isiyo na mfano wake<br />

(v) Ndoa yake na Bibi Khadija<br />

(vi) Kuchukia maovu na kujitenga pangoni<br />

(i) Kuzaliwa Makka katika kabila la Quraish<br />

Mtume (s.a.w) kuzaliwa Makkah katika kabila tukufu la<br />

Quraysh, chini ya ulezi wa Babu yake Abdul-Muttalib, aliyekuwa<br />

kiongozi wa Maquraysh, ni kielelezo kuwa alistahiki kuchaguliwa<br />

kuwa kiongozi wa watu wake. Kabila la Quraish ni katika kizazi cha<br />

Nabii Ibrahim (a.s) kupitia kwa Ismail (a.s). Mtume (s.a.w) kuwa<br />

Mtume na kiongozi wa Dola ya Kiislamu ni jibu la dua ya Nabii<br />

Ibrahimu baada ya kukamilisha kazi ya kujenga upya Ka’abah:<br />

Na (kumbukeni khabari hii pia) Ibrahimu alipoinua kuta<br />

za nyumba (hii ya Al-Kaaba) na Ismail (pia); (wakaomba<br />

41

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!