08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Hadith hii pia inamuhimiza Muislamu kumsaidia ndugu<br />

yake aliyedhulumiwa mpaka apate haki yake.<br />

Haya yote tuliyoyaorodhesha, ikiwa ni kushauriana na<br />

kusaidiana wakati wa matatizo, kutekelezeana wajibu,<br />

kuchangamkiana, kupeana zawadi, kuzuia kinachodhuru kisimfike<br />

ndugu yako, kumsaidia mwenye kudhulumiwa, kupeana ushauri<br />

mzuri, kukatazana maovu, n.k. ni miongoni mwa mambo mema<br />

ambayo wanakundi wanatakiwa wajizatiti katika kutendeana ili<br />

kuhuisha na kudumisha udugu na upendo miongoni mwao na<br />

miongoni mwa Waislamu wote kwa ujumla; upendo utakao<br />

wawezesha kushikamana pamoja katika kuhuisha na kusimamisha<br />

dini ya Allah (s.w) kama tunavyoamrishwa:<br />

Na shikamaneni kwa kamba (dini) ya Allah nyote, wala<br />

msiachane. Na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu iliyo<br />

juu yenu. (Zamani) mlikuwa maadui; naye akaziunganisha<br />

nyoyo zenu; hivyo kwa neema yake mkawa ndugu. Na<br />

mlikuwa ukingoni mwa shimo la moto (wa Jahannam), naye<br />

akakuokoeni nalo. Namna hivi Mwenyezi Mungu<br />

anakubainishieni aya zake ili mpate kuongoka. (3:103)<br />

Pamoja na aya hii kuwaamrisha Waislamu washikamane<br />

pamoja katika kuipigania Dini ya Allah, inatuelekeza vile vile<br />

turejee historia tuone jinsi gani lile kundi la Waislamu lililokuwa<br />

pamoja na Mtume (s.a.w) lilivyoshikamana kwa udugu na upendo<br />

baada ya kuwa Waislamu. Historia inatufahamisha kuwa kabla ya<br />

92

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!