08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

umuhimu wa watu kuisoma Qur’an, kuielewa, kuizingatia,<br />

kuifundisha na kuitekeleza. Zipo Hadith nyingi, hatuna haja ya<br />

kuzinukuu.<br />

Marekani kwa kupitia aliyekuwa Waziri wa Mambo ya nchi<br />

za nje wa zamani Bw. Collin Powell, na Waziri wa Ulinzi Bwana<br />

Donald Rumsfed wamesema kuwa umadhubuti wa Waislamu<br />

unatokana na wao kuisoma, kuifundisha, kuiamini na kuifuata<br />

Qur’an. Hivyo ufumbuzi wa kudumu ni kuwatoa Waislamu katika<br />

Uislamu wao kwa kuingilia mafundisho ya Qur’an. Na njia nzuri ni<br />

kuanzia kwenye madrasa zao. Kampeni hiyo iwe dunia nzima.<br />

Hapa tutaangalia tu wanayoyafanya Tanzania na mafanikio yao<br />

ukilinganisha na yetu sisi wanaharakati.<br />

Njia ya kwanza waliona ni kutoa misaada kwenye madrasa<br />

ili iwe ni mwanya na hatimaye kubadilisha mitaala ya madrasa.<br />

Huko Kenya wakaenda kwa pupa kwa balozi wa Marekani kutoa<br />

rundo la misaada ya vitabu na pesa kwa madrasa. Waislamu<br />

wakashituka na wakakataa. Makafiri hawakukata tamaa<br />

wakajifunza kosa lao. Hapa Tanzania, wakaamua kuwa kwanza<br />

kabisa waanze na utafiti utakaowajulisha ukweli halisi juu ya<br />

madrasa. Na wakaona Marekani wasionekane waziwazi.<br />

Wakawatumia watu wengine, yaani shirika la Kijerumani liitwalo<br />

Konrad Adeneur Stiftung. Mwezi Mei/Juni 2003 walifanya<br />

utafiti wao waliouita “Qur’an Madrasa Baseline Survey.”<br />

Yaani utafiti wenye lengo la kujua hali halisi ya Madrasa kwa mkoa<br />

wa Dar es Salaam. Waliyagundua mengi, lakini kwa sasa tuseme tu<br />

kuwa baadhi ya waliyoyajua ni kuwa karibu nusu ya walimu wa<br />

madrasa wanapata mshahara wa chini ya shilingi 10’000/= kwa<br />

mwezi. Na wengine hawalipwi kabisa. Theluthi mbili ya madrasa<br />

zinamilikiwa na watu binafsi na zipo vibarazani. Wazazi na<br />

viongozi wa Kiislamu hawana taarifa wala hawataki kufuatilia<br />

kinachoendelea kwenye hizo madrasa. Baada ya kuupata ukweli<br />

huo Marekani ikaamua kuanza kuingilia madrasa kwa kuanzia<br />

Zanzibar.<br />

32

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!