Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
umuhimu wa watu kuisoma Qur’an, kuielewa, kuizingatia,<br />
kuifundisha na kuitekeleza. Zipo Hadith nyingi, hatuna haja ya<br />
kuzinukuu.<br />
Marekani kwa kupitia aliyekuwa Waziri wa Mambo ya nchi<br />
za nje wa zamani Bw. Collin Powell, na Waziri wa Ulinzi Bwana<br />
Donald Rumsfed wamesema kuwa umadhubuti wa Waislamu<br />
unatokana na wao kuisoma, kuifundisha, kuiamini na kuifuata<br />
Qur’an. Hivyo ufumbuzi wa kudumu ni kuwatoa Waislamu katika<br />
Uislamu wao kwa kuingilia mafundisho ya Qur’an. Na njia nzuri ni<br />
kuanzia kwenye madrasa zao. Kampeni hiyo iwe dunia nzima.<br />
Hapa tutaangalia tu wanayoyafanya Tanzania na mafanikio yao<br />
ukilinganisha na yetu sisi wanaharakati.<br />
Njia ya kwanza waliona ni kutoa misaada kwenye madrasa<br />
ili iwe ni mwanya na hatimaye kubadilisha mitaala ya madrasa.<br />
Huko Kenya wakaenda kwa pupa kwa balozi wa Marekani kutoa<br />
rundo la misaada ya vitabu na pesa kwa madrasa. Waislamu<br />
wakashituka na wakakataa. Makafiri hawakukata tamaa<br />
wakajifunza kosa lao. Hapa Tanzania, wakaamua kuwa kwanza<br />
kabisa waanze na utafiti utakaowajulisha ukweli halisi juu ya<br />
madrasa. Na wakaona Marekani wasionekane waziwazi.<br />
Wakawatumia watu wengine, yaani shirika la Kijerumani liitwalo<br />
Konrad Adeneur Stiftung. Mwezi Mei/Juni 2003 walifanya<br />
utafiti wao waliouita “Qur’an Madrasa Baseline Survey.”<br />
Yaani utafiti wenye lengo la kujua hali halisi ya Madrasa kwa mkoa<br />
wa Dar es Salaam. Waliyagundua mengi, lakini kwa sasa tuseme tu<br />
kuwa baadhi ya waliyoyajua ni kuwa karibu nusu ya walimu wa<br />
madrasa wanapata mshahara wa chini ya shilingi 10’000/= kwa<br />
mwezi. Na wengine hawalipwi kabisa. Theluthi mbili ya madrasa<br />
zinamilikiwa na watu binafsi na zipo vibarazani. Wazazi na<br />
viongozi wa Kiislamu hawana taarifa wala hawataki kufuatilia<br />
kinachoendelea kwenye hizo madrasa. Baada ya kuupata ukweli<br />
huo Marekani ikaamua kuanza kuingilia madrasa kwa kuanzia<br />
Zanzibar.<br />
32