08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Utangulizi<br />

DHANNA YA KUHUISHA UISLAMU<br />

KATIKA JAMII<br />

Tunaposema kuhuisha Uislamu katika jamii hatuna maana ya<br />

kuongeza idadi ya Waislamu katika jamii. Waislamu wanaweza<br />

kuwa asilimia 99.99 lakini bado Uislamu usiwepo katika jamii.<br />

Kwa mfano nchi nyingi za Uarabuni ikiwemo Saudi Arabia ilipo<br />

Ka’abah, idadi kubwa ya wakazi wa nchi hizo, zaidi ya asilimia 99<br />

ni Waislamu lakini bado Uislamu haujasimama katika nchi hizo.<br />

Tusiende mbali, turudi hapa Tanzania, asilimia 99 na zaidi ya<br />

wakazi wa Zanzibar ni Waislamu. Vile vile hapa Tanzania kuna<br />

idadi kubwa ya Waislamu ukilinganisha na watu wengine katika<br />

mikoa yote ya Pwani, Tabora na Kigoma. Aidha, idadi ya Waislamu<br />

ni kubwa sana takribani katika miji yote mikubwa ya mikoa ya<br />

Tanzania; kielelezo ni wingi wa misikiti katika miji hiyo na<br />

kufurika kwake katika siku za Ijumaa na hasa katika mwezi wa<br />

Ramadhani, lakini bado kijamii hapaoneshi kuwepo Uislamu<br />

katika mikoa na miji hiyo ya Waislamu.<br />

Kinyume chake, Waislamu wanaweza kuwa wachache katika jamii<br />

kama asilimia (10%) tu hivi lakini bado wakaweza kudhihirisha<br />

Uislamu katika jamii yao. Mhadhiri maarufu wa “Biblia” duniani<br />

(wa ulinganisho wa Uislamu na Ukristo) duniani Al-marhuum<br />

Sheikh, Ahmed Deedat, wa Afrika ya Kusini, alishangazwa sana na<br />

hali ya Waislamu wa Tanzania, alipotembelea hapa mwaka 1981.<br />

Alishangaa kuona kuwa pamoja na wingi wa Waislamu, hasa<br />

Zanzibar, Uislamu haukuwa na athari yoyote katika jamii. Kwa<br />

mfano, wakati Sheikh Deedat anaonesha mshangao wake,<br />

alishikilia gazeti la “Daily News” lililokuwa na orodha ya<br />

wanaojiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo cha Ardhi na<br />

Chuo cha Maji. Alionesha kuwa katika wale wote waliochaguliwa<br />

kujiunga na Vyuo hivyo Waislamu walikuwa chini ya<br />

(x)

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!