08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

(i) Mtu binafsi kusoma elimu sahihi juu ya Uislamu kwa<br />

kufuata mtaala wa: Maarifa ya Uislamu, Darasa la Watu<br />

Wazima, Juzuu 1-7 (IPC).<br />

(ii) Mtu binafsi kujipamba na Sifa za Mwanaharakati<br />

(kuingiza elimu sahihi katika matendo).<br />

(iii) Kuiendea familia - mke/mume, watoto, wazazi na wale<br />

wote waliochini a malezi ya familia.<br />

(iv) Kuwafikishia ujumbe wa Uislamu marafiki na jamaa wa<br />

karibu na kuwashawishi nao waufikishe ujumbe huo kwa<br />

familia zao, rafiki na jamaa zao wa karibu.<br />

(v) Kuanzisha Darasa Duara litakalo wakusanya na<br />

kuwaelimisha juu ya Uislamu kinadharia na kimatendo<br />

wale wote uliowalingania na kuupokea ujumbe wa<br />

Uislamu. Darasa Duara likiendeshwa na<br />

kuongozwa inavyostahiki huwa ndio chimbuko la kundi<br />

madhubuti la Harakati.Darasa Duara huanzia ngazi ya<br />

familia kisha mtaa hadi kufikia ngazi ya taifa kulingana na<br />

ukuaji wakundi la Harakati.<br />

Nini Darasa Duara?<br />

Darasa Duara ni darasa linaloendeshwa kwa mtindo wa<br />

semina. Panakuwa na mada inayowasilishwa na mmoja wa wana<br />

darasa au kiongozi wa darasa, kisha mada hiyo huchangiwa na<br />

kujadiliwa na wanadarasa mpaka ieleweke vyema kwa kila mwana<br />

darasa. Baada ya mada kueleweka. Wanadarasa hupitisha<br />

maazimio ya utekelezaji wa mada hiyo katika maisha ya kila siku.<br />

Kisha kufuatia tathmini ya utekelezaji wa maazimio haya katika<br />

darasa linalofuata kabla ya kuanza mada mpya. Hivi ndivyo Mtume<br />

(s.a.w) alivyowalea maswahaba zake kama tunavyojifunza kwa Ibn<br />

Masoud kuwa, wao (Maswahaba) hawakuwa wanapokea aya kumi<br />

mpya alizokuwa akiwasomea Mtume (s.a.w) kabla<br />

hawajahakikisha zile kumi walizosomewa awali wameziingiza<br />

katika matendo ya maisha yao ya kila siku. Mtume (s.a.w) naye<br />

alikuwa makini katika kufuatilia utekelezaji wa yale aliyowafunza<br />

maswahaba wake.<br />

109

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!