Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
(i) Mtu binafsi kusoma elimu sahihi juu ya Uislamu kwa<br />
kufuata mtaala wa: Maarifa ya Uislamu, Darasa la Watu<br />
Wazima, Juzuu 1-7 (IPC).<br />
(ii) Mtu binafsi kujipamba na Sifa za Mwanaharakati<br />
(kuingiza elimu sahihi katika matendo).<br />
(iii) Kuiendea familia - mke/mume, watoto, wazazi na wale<br />
wote waliochini a malezi ya familia.<br />
(iv) Kuwafikishia ujumbe wa Uislamu marafiki na jamaa wa<br />
karibu na kuwashawishi nao waufikishe ujumbe huo kwa<br />
familia zao, rafiki na jamaa zao wa karibu.<br />
(v) Kuanzisha Darasa Duara litakalo wakusanya na<br />
kuwaelimisha juu ya Uislamu kinadharia na kimatendo<br />
wale wote uliowalingania na kuupokea ujumbe wa<br />
Uislamu. Darasa Duara likiendeshwa na<br />
kuongozwa inavyostahiki huwa ndio chimbuko la kundi<br />
madhubuti la Harakati.Darasa Duara huanzia ngazi ya<br />
familia kisha mtaa hadi kufikia ngazi ya taifa kulingana na<br />
ukuaji wakundi la Harakati.<br />
Nini Darasa Duara?<br />
Darasa Duara ni darasa linaloendeshwa kwa mtindo wa<br />
semina. Panakuwa na mada inayowasilishwa na mmoja wa wana<br />
darasa au kiongozi wa darasa, kisha mada hiyo huchangiwa na<br />
kujadiliwa na wanadarasa mpaka ieleweke vyema kwa kila mwana<br />
darasa. Baada ya mada kueleweka. Wanadarasa hupitisha<br />
maazimio ya utekelezaji wa mada hiyo katika maisha ya kila siku.<br />
Kisha kufuatia tathmini ya utekelezaji wa maazimio haya katika<br />
darasa linalofuata kabla ya kuanza mada mpya. Hivi ndivyo Mtume<br />
(s.a.w) alivyowalea maswahaba zake kama tunavyojifunza kwa Ibn<br />
Masoud kuwa, wao (Maswahaba) hawakuwa wanapokea aya kumi<br />
mpya alizokuwa akiwasomea Mtume (s.a.w) kabla<br />
hawajahakikisha zile kumi walizosomewa awali wameziingiza<br />
katika matendo ya maisha yao ya kila siku. Mtume (s.a.w) naye<br />
alikuwa makini katika kufuatilia utekelezaji wa yale aliyowafunza<br />
maswahaba wake.<br />
109