Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
itajiangamiza yenyewe kwa ufuska utakaotokea. Ni hila hiyo ya<br />
shetani ndiyo inayowapelekea baadhi ya watu kudhani kuwa<br />
maendeleo hayawezi kupatikana sharti kwanza wanawake watupe<br />
shungi zao na hijabu. Na ili kuyaweka mawazo vizuri kabla ya<br />
kujadiliana mambo muhimu ya kitaifa baadhi ya vikao<br />
hutanguliwa na vikundi vya wanawake walionusu uchi wakinengua<br />
jukwaani!<br />
Tano, Binaadamu kwa umbile lake hayuko tayari kukubali<br />
kirahisi wito wa kufanya maovu. Kwa sababu hiyo siku zote jambo<br />
hata likiwa ovu hupambwa kwa sifa nzuri na ndipo watu hulitenda.<br />
Hata kama imethibitika kuwa pombe inaharibu afya ya mwili na<br />
akili na hivyo kudidimiza jamii, matangazo ya pombe katu<br />
hayasemi: Kunywa pombe ili uharibu haraka afya yako ya mwili na<br />
akili, bali yatasema: “Baada ya kazi ngumu burudisha mwili wako<br />
kwa pombe kadhaa ili uwe mwenye afya, nguvu na furaha tele!”<br />
Hizi ni hila za shetani.<br />
Sita, Binaadamu kwa umbile lake pia anatamani sana<br />
kufikia daraja ya juu kuliko aliyonayo sasa, au kutamani kudumu<br />
milele. Ndiyo maana Shetani alimdanganya, Nabii Adamu (a.s)<br />
kuwa atakuwa Malaika na ataishi milele akiiasi amri ya Allah(s.w).<br />
Hila hiyo hiyo yaendelea kutuumiza hata leo kwani shetani<br />
huwarubuni watu kwa kuwafanya waamini kuwa<br />
yanayopendekezwa na shetani kama wizi, dhuluma, mauaji, riba,<br />
n.k. yatawapatia maisha ya juu ya anasa na fahari.<br />
Saba, Binadamu anapomwasi Allah (s.w), Allah (s.w)<br />
humwumbua na kuyaweka wazi maovu yake.<br />
166