08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

itajiangamiza yenyewe kwa ufuska utakaotokea. Ni hila hiyo ya<br />

shetani ndiyo inayowapelekea baadhi ya watu kudhani kuwa<br />

maendeleo hayawezi kupatikana sharti kwanza wanawake watupe<br />

shungi zao na hijabu. Na ili kuyaweka mawazo vizuri kabla ya<br />

kujadiliana mambo muhimu ya kitaifa baadhi ya vikao<br />

hutanguliwa na vikundi vya wanawake walionusu uchi wakinengua<br />

jukwaani!<br />

Tano, Binaadamu kwa umbile lake hayuko tayari kukubali<br />

kirahisi wito wa kufanya maovu. Kwa sababu hiyo siku zote jambo<br />

hata likiwa ovu hupambwa kwa sifa nzuri na ndipo watu hulitenda.<br />

Hata kama imethibitika kuwa pombe inaharibu afya ya mwili na<br />

akili na hivyo kudidimiza jamii, matangazo ya pombe katu<br />

hayasemi: Kunywa pombe ili uharibu haraka afya yako ya mwili na<br />

akili, bali yatasema: “Baada ya kazi ngumu burudisha mwili wako<br />

kwa pombe kadhaa ili uwe mwenye afya, nguvu na furaha tele!”<br />

Hizi ni hila za shetani.<br />

Sita, Binaadamu kwa umbile lake pia anatamani sana<br />

kufikia daraja ya juu kuliko aliyonayo sasa, au kutamani kudumu<br />

milele. Ndiyo maana Shetani alimdanganya, Nabii Adamu (a.s)<br />

kuwa atakuwa Malaika na ataishi milele akiiasi amri ya Allah(s.w).<br />

Hila hiyo hiyo yaendelea kutuumiza hata leo kwani shetani<br />

huwarubuni watu kwa kuwafanya waamini kuwa<br />

yanayopendekezwa na shetani kama wizi, dhuluma, mauaji, riba,<br />

n.k. yatawapatia maisha ya juu ya anasa na fahari.<br />

Saba, Binadamu anapomwasi Allah (s.w), Allah (s.w)<br />

humwumbua na kuyaweka wazi maovu yake.<br />

166

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!