Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Mzigo uliovunja mgongo wa Muhammad (s.a.w) kipindi<br />
kile si mwingine ila ile hali ya udhalimu na uovu iliyoshamiri katika<br />
jamii yake. Alikuwa na ari kubwa ya kuiondoa ile hali na<br />
kusimamisha uadilifu katika jamii lakini hakujua ni vipi<br />
atafanikisha hilo.<br />
Mafunzo yatokanayo na maandalizi ya ki-il-hamu<br />
Kutokana na matukio haya yanayoashiria kuandaliwa kwa<br />
Mtume (s.a.w) kabla ya kupewa Utume rasmi, tunajifunza kuwa<br />
katika kuhuisha na kusimamisha Uislamu katika jamii hatuna budi<br />
kuzingatia haya yafuatayo:<br />
Kwanza, hatunabudi kuwaandaa watoto wetu kuwa<br />
Makhalifa wa Allah (s.w) mapema kabla hata hawajazaliwa.<br />
Maandalizi haya yanawezekana pale wazazi wote wawili<br />
watakapokuwa na mtazamo huo wa Ukhalifa. Kisha baada ya<br />
watoto kuzaliwa tuwaadhinie na kuwakimia,tuwafanyie aqika na<br />
kuwapa majina mazuri, tuwalee kwa mapenzi na huruma na<br />
kuwafunza tabia njema tangu wangali wachanga. Tuwasomeshe<br />
watoto wetu katika shule na vyuo vyenye kufuata mfumo wa elimu<br />
wa Kiislamu wenye lengo la kuandaa Makhalifa wa Allah(s.w).<br />
Pili, hatunabudi kuandaa Waalimu na Madaiyah watakao<br />
fundisha Uislamu na taaluma nyingine kwa lengo la kusimamisha<br />
Ukhalifa katika jamii.<br />
Tatu, Mume na Mke (Baba na Mama) katika familia<br />
hawanabudi kushirikiana na kusaidiana kwa huruma na mapenzi<br />
ili kupata uwezo wa kuwalea watoto vilivyo na kupata wasaa wa<br />
kuyaendea masuala ya jamii.<br />
Nne, Wanawake wa Kiislamu, hawanabudi kumfanya Bibi<br />
Khadijah, Mkewe Mtume (s.a.w), kuwa kiigizo chao katika<br />
kuwasaidia na kuwaliwaza waume zao hasa wanapokuwa katika<br />
harakati za kuhuisha na kusimamisha Uislamu katika jamii.<br />
48