Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Kundi la Harakati halina budi kuwa macho sana, kwani ni<br />
rahisi mno kutumbukia ndani ya majivuno na kujifaharisha. Ni<br />
rahisi kwa wale Waislamu wachache katika jamii wanaojizatiti<br />
kufanya amali njema, kujiona kuwa wao ni bora kuliko jamii<br />
iliyowazunguka. Pia wale wanaojitahidi kutenda mema na<br />
kuwafanyia wengine mema, hutokea kuwa watu hufurahia<br />
mwenendo wao na kuanza kuwasifu. Sifa hizi huwapandisha<br />
kichwa na kujiona kuwa ni watu muhimu, wakaanza kuwatangazia<br />
watu kuwa wao ni muhimu na wakajionyesha katika mwendo wao.<br />
Kundi la Harakati litakapotumbukia katika majivuno na<br />
kujifaharisha, lifahamu kuwa limeshashindwa na kazi na badala ya<br />
kutarajia kutengenekewa, litarajie kuharibikiwa na kuhiliki. Kundi<br />
la Harakati litaepukana na majivuno na kujitukuza endapo kila<br />
Mwanaharakati na kundi la Harakati kwa ujumla, litajitahidi<br />
kufanya yafuatayo:<br />
kwanza, kuwa na Ikhlas – kufanya kazi ya Da’awah kwa<br />
ajili ya Allah (s.w) tu kwa kutarajia kupata Radhi yake na malipo<br />
bora ya Akhera.<br />
Pili, kila Mwanaharakati na kundi la Harakati kwa ujumla<br />
lijifanyie muhasaba (lijihesabu na kujitathmini). Muislamu<br />
mwenye tabia ya kujihesabu kabla ya kuhesabiwa hujigundua<br />
udhaifu wake na makosa yake. Mtu mwenye kujiona makosa yake<br />
na udhaifu wake mara kwa mara kamwe hawezi kujiona bora na wa<br />
maana kuliko wengine. Daima atajiona si lolote wala si chochote<br />
mbele ya wengine na mbele ya Allah (s.w) na atajitahidi kutembea<br />
kwa unyenyekevu katika ardhi.<br />
Tatu, jambo linalosaidia sana katika kumuepusha Muislamu<br />
na majivuno na kujitukuza katika ardhi, ni kujenga tabia ya<br />
kuwaangalia watu wema na wacha-Mungu waliomzidi katika<br />
kutenda wema. Muislamu atakapojilinganisha na watu watendao<br />
105