08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

hakilaumiwi kwa kuonesha alama ya uchafu usoni. Ni juu ya<br />

mwenye kujitazama kiooni (mkosolewaji) kuundoa uchafu huo<br />

usoni mwake.<br />

6. Kujiepusha na kujiona<br />

Kujiona na majivuno ni miongoni mwa vipengele vya tabia<br />

ambayo humtoa mtu katika njia ya Allah (s.w). Makemeo ya Allah<br />

(s.w) yako wazi juu ya wenye kujiona na kujivuna katika ardhi.<br />

Hebu turejee aya chache zifuatazo:<br />

Wala usiwatazame (watu) kwa upande mmoja wa uso, wala<br />

usiende katika nchi kwa maringo, hakika Mwenyezi Mungu<br />

hampendi kila ajivunaye, ajifaharishaye. (31:18)<br />

Wala usitembee(usiende)katika ardhi kwa maringo. Hakika<br />

wewe huwezi kupasua ardhi wala huwezi kufikia urefu wa<br />

milima(Basi unajivuna nini). (17:37).<br />

Aya hizi zinatufahamisha wazi kuwa Allah (s.w) hawapendi<br />

wanaojivuna na kujifaharisha. Hivyo mwenye tabia hii mbaya hana<br />

radhi mbele ya Allah (s.w) katika maisha haya ya dunia na katika<br />

maisha ya Akhera.<br />

Mwanaharakati na kundi la Harakati kwa ujumla, ili lipate<br />

mafanikio katika kazi yake ya kulingania na kusimamisha Uislamu<br />

katika jamii halina budi kujiepusha na kila aina ya kiburi. Pasiwe<br />

na namna yeyote ile ya kujiona kuwa wao ni bora kuliko wengine<br />

wala wasijivunie mafaniko yoyote watakayopata.<br />

104

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!