08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Na (Mwenyezi Mungu) akamfundisha (Nabii) Adam majina ya vitu vyote,<br />

kisha Akaviweka mbele ya Malaika, na Akasema (kuwaambia Malaika):<br />

“Niambieni majina ya vitu hivi ikiwa mnasema kweli (kuwa nyinyi ndio<br />

wajuzi wa mambo)”. Wakasema (Malaika): “Utakatifu ni Wako! Hatuna<br />

ilimu isipokuwa ile Uliyotufundisha; bila shaka Wewe ndiye Mjuzi na<br />

ndiye Mwenye hikima.” Akasema (Mwenyezi Mungu): “Ewe Adam!<br />

Waambie majina yake”. Alipowaambia majina yake alisema (Mwenyezi<br />

Mungu): “Sikukwambieni kwamba Mimi ninajua siri za mbinguni na za<br />

ardhi; tena najua mnayoyadhihirisha na mliyokuwa mnayaficha?” Na<br />

(wakumbushe watu khabari hii): Tulipowaambia Malaika: “Msujudieni<br />

Adam;” (yaani mwadhimisheni kwa ile ilimu yake aliyopewa).<br />

Wakamsujudia wote isipokuwa Iblis, akakataa na akajivuna; na (tokea<br />

hapo) alikuwa katika makafiri” (2:31-34).<br />

Mbinu za kumuandaa Khalifa<br />

Zipo mbinu kadhaa za kuwaandaa wanafunzi Waislamu wainukie<br />

kuwa Makhalifa wa Allah (s.w) (watawala wa jamii kwa niaba ya Allah (s.w)).<br />

Baadhi ya mbinu hizo ni hizi zifuatazo:<br />

(i) Kuliweka bayana lengo la Elimu.<br />

(ii) Kutumia lugha nyepesi inayofahamika kwa mwanafunzi.<br />

(iii) Kufafanua somo/mada kwa Aya na Hadith.<br />

(iv) Kutoa na kutumia mifano na vielelezo vya Kiislamu.<br />

(v) Kuleta Mazingatio ya Allah (s.w) kupitia mada mbali mbali za<br />

elimu ya mazingira.<br />

(vi) Kukosoa nadharia potofu.<br />

210

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!