08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

dhalimu kwa sababu ametunukiwa vipaji mbalimbali vya akili,<br />

utambuzi binafsi (self consciousness) wa hali ya juu, elimu na<br />

Uhuru wa kufanya alitakalo pamoja na neema nyingine mbali<br />

mbali kama Allah (s.w) anavyoainisha katika aya mbali mbali za<br />

Qur’an zikiwemo zifuatazo:<br />

“Na hakika Tumewatukuza wanaadamu na tukawapa vya<br />

kupanda barani na baharini na Tumewaruzuku vitu vizuri<br />

vizuri, na Tumewatukuza kuliko wengi katika wale<br />

Tuliowaumba, kwa utukufu ulio mkubwa (kabisa).” (17:70)<br />

“Hakika Tumemuumba mwanaadamu kwa umbo lililo bora<br />

kabisa” (95:4)<br />

“Yeye ndiye aliyekuumbieni vyote vilivyomo katika ardhi<br />

(kabla hajakuumbeni ili mkute kila kitu tayari), tena<br />

akakusudia kuumba mbingu; na akazifanya mbingu saba.<br />

Naye ndiye ajuaye kila kitu”. (2:29)<br />

Mwanaadamu amekirimiwa na Mola wake vipaji na neema<br />

nyingine kuliko viumbe wengine, ikiwemo mbingu, ardhi na<br />

milima (majabali), ili aweze kubeba amana ya kusimamisha<br />

Uislamu katika jamii. Mwanaadamu atakapo amua kuvitumia<br />

vipaji na neema hizo kwa kufikia malengo mengine kinyume na<br />

kusimamisha Ukhalifa wa Allah (s.w) katika ardhi, atakuwa mwizi<br />

wa fadhila na atakuwa hamdhulumu yeyote ila nafsi yake.<br />

118

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!